RUVUMA
kamishna wa kodi za ndani kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) BW. Alfred Mregi amefanya ziara ya kuwatembelea wafanyabiashara wilayani
tunduru mkoani Ruvuma katika maeneo yao ya biashara lengo likiwa ni kusikiliza
maoni ,ushauri, na changamoto zinazowakumba wafanyabiashara wilayani humu katika maeneo yao ya biashara
sambamba na hilo Bw. Mregi amefanya kikao na wafanyabiashara wa
wilaya ya Tunduru ambapo timu ya wataalamu
kutoka TRA walitoa elimu ya kodi
kwa wafanyabiashara na baadae Kamishna aliweza kusiliza changamoto pamoja na
maoni kutoka kwa wafanyabiashara.
Katika kikao hicho changamoto mbalimbali zimetolewa na wafanyabiashara kuhusiana na
kodi ambapo changamoto hizo zimetatuliwa kwa kutolewa ufafanuzi na kamshina wa
kodi za ndani,
Pamoja na hayo Bw. Alfred Mregi amewaomba na kuwasisitiza
wafanyabiashara wilayani Tunduru kufuata sheria zilizowekwa na serikali
ili waweze kuondokana na changamoto za kikodi pamoja na kuepuka uonevu unaoweza
kujitokeza kwa kutokujua sheria zinasemaje.
pia amewaomba wafanyabiashara kuendelea kutoa ushirikiano kwa
Mamlaka ya Mapato Tanzania wilayani humo kwa kushiriki semina ili waweze kujifunza ni kwa namna gani
sheria zinawataka wafanye aidha amesema TRA itaendelea kutoa semina na elimu ya
kodi mara kwa mara ili kuwawezesha wafanyabiashara kusikilizwa na kupaia elimu
ya kodi





No comments:
Post a Comment