Takriban
vikundi 55 vya maendeleo kutoka kata 18 ndani ya Halmashauri ya Wilaya
ya Songea, mkoani Ruvuma, vinatarajiwa kunufaika na mashine za kuongeza thamani
ya zao la mahindi zitakazotolewa na Shirika la Kiserikali la Uturuki (TIKA).
Katika
ufadhili huo, vikundi 23 vitapokea mashine za kusaga na kukoboa
mahindi, huku vikundi 32 vikipewa mashine za kupukuchua mahindi.
Filiz
Sahinci, Mratibu wa Programu za TIKA nchini
Tanzania, akizungumza katika ziara ya kutembelea vikundi hivyo, amesema moja ya
malengo ya shirika hilo ni kuwawezesha wananchi wa hali ya chini kiuchumi kwa
kuwasaidia katika changamoto mbalimbali zinazowakwamisha kiuchumi hasa wakiwa
wamelilenga kundi la wanawake, amesema kuwa “Mwanamke akiwa na nguvu ya
kiuchumi, jamii nzima itakuwa na uchumi imara.”
Kwa
upande wake, Mbunge wa Jimbo la Peramiho ambaye pia ni Waziri wa Afya, Mhe.
Jenista Mhagama, amelipongeza shirika la TIKA kwa kuendelea kushirikiana na
Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuleta
maendeleo kwa wananchi wa Tanzania.
Mhe.
Mhagama ametoatoa wito kwa wananchi wanaonufaika na mashine hizo kuendelea
kujikita katika uzalishaji wa mazao na kuzitumia vyema fursa walizopata ili
kujikwamua kiuchumi.
Naye
Thomasi Maswolwa, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema
jitihada za kuwatafutia wananchi wadau wa maendeleo ni utekelezaji wa Ilani ya
Uchaguzi ya CCM. Ambapo pia amesisitiza umuhimu wa kutunza amani na utulivu
uliopo nchini ambao umewezesha ushirikiano wa kimataifa kama huu kutoka TIKA.
Wananchi waliopokea msaada huo wamelishukuru shirika la TIKA na Ofisi ya Mbunge kwa kutambua umuhimu wa vikundi vya maendeleo. Walisema msaada huo utasaidia sana vikundi na wanachama mmoja mmoja katika kujikwamua kiuchumi na kuongeza thamani ya mazao yao, hasa mahindi.





No comments:
Post a Comment