Tuesday, 1 July 2025

KADA WA CCM TULIZO MAPUNDA AREJESHA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA MBINGA VIJIJINI

 

Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tulizo Mapunda, amekamilisha hatua ya awali ya mchakato wa kuwania nafasi ya ubunge kwa kurejesha rasmi fomu ya kugombea katika ofisi ya CCM Wilaya ya Mbinga.

Mapunda alichukua fomu hiyo tarehe 29 Juni 2025, ikiwa ni sehemu ya mchakato wa ndani wa chama cha CCM wa kuwapata wagombea watakaowania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu ujao.

Mapunda anawania  kupitishwa na chama chake ili kupeperusha bendera ya CCM kwa nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini.

Leo, tarehe 01 Julai 2025, Mapunda amerudisha rasmi fomu hiyo, hatua inayodhihirisha dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Jimbo la Mbinga Vijijini endapo atapewa ridhaa na chama na hatimaye kushinda uchaguzi.

Akizungumza mara baada ya kurejesha fomu hiyo, Mapunda amewashukuru wanachama wa CCM pamoja na wananchi wa Jimbo la Mbinga Vijijini kwa ushirikiano waliompa tangu mwanzo wa safari yake ya kisiasa

Amesema  kuwa ana nia thabiti ya kuleta maendeleo kwa kushirikiana na wananchi, endapo atapewa nafasi ya kuwa Mbunge wa jimbo hilo.

No comments:

Post a Comment