Wednesday, 5 July 2017

Timbulo amchana mpenzi wake wa zamani


Haijawa kitu rahisi kwa mbongo Fleva Ally Timbulo a.k.a Timbulo kushawishika na maneno ya Mpenzi wake wazamani (Ex Girl Friend) ambaye anatamani iwe kama zamani ambapo jamaa ameamua kumchana kwa kumtolea ngoma inayojulikana kwa jina la Mshuma

 “Nimemuimbia EX wangu aliyeniacha , kunikimbia, aliyeniona si kitu na kunitafuta  kutaka turudiane” alisema Timbulo wakati akitambulisha wimbo wake mpya kwenye kipindi cha (Xtra Xtra Large) (XXL) Kubwa kubwa kuliko kinachorushwa na The People Station Clouds Fm.

Pia Timbilo amewasihi mashabiki wake kutokuwa na hofu dhidi ya mtindo wake mpya wa kutoa nyimbo mfululizo na kusema haofii kukandamiza nyimbo nyingine.

Sikandamizi miziki wangu nawapa mashabiki wanachokitaka”

Ikumbukwe Miezi micha iliyopita Timbulo aliachia ngoma ya Mfuasi pindi ikiwa inafanya vizuri  katika soko la muziki na masikioni mwa watu akaachia ngoma  ya Ni wewe na pindi ikiwa niaanza kueleweka kwa mashabiki ameudondosha ngoma ya Mshumaa.

No comments:

Post a Comment