Thursday, 13 July 2017

DAGE wamuomba waziri muhagama kuwanunulia mashine zitakazo wawezesha kufanya kazi kirahisi

Chama cha wabunifu na watengenezaji wa vifaa mbalimbali vya walemavu(DAGE),kimemwomba Waziri waSera,Bunge,Kazi Ajira, Vijana na Walemavu Jenista Mhagama,kuwa nunulia mashine za kutengenezea maumbo mbali mbali ya vifaa vya walemavu.

Ombi hilo lilitolewa jana na Katibu Mtendaji  wa chama hicho Patrick Mdachi, ambapo alisema mashine walionayo kwa sasa ni ya zamani na haina uwezo wakutengeneza baiskeli 35 kwa mwezi.

“Kwa kipindi kirefu tumekuwa tuki pata shida wakati watu wanapo kuja kuleta tenda ya kuwa tengenezea baiskeli za aina tofauti tofauti za walemavu ambapo tunashindwa kutengeneza kwa haraka na mashine hiyo imechoka alisema.”Mdachi

Alisema mashine hiyo inazaidi ya miaka 10 tangu ianze kufanya kazi na wakati mwingine wanalazimika kuitengeneza ili iweze kufanya kazi.

Mdachi alisema kutokana tatizo hilo   wamekuwa wakishindwa kutengeneza baiskeli nyingi ambazo zinauhitaji mkubwa kwa baadhi ya walemavu.

“kwa  kipindi cha cha nyuma kwa  mwezi mmoja tulikuwa tunatengezena  baiskeli 35 kiasi lakini sasa tunashindwa kufikia kiwango hicho kutokana na mashine hiyo kusumbua alisema,”Mdachi

Pia alisema kumekuwepo na wimbi la baadhi ya mafundi mitaani wanaowatengenezea walemavu baiskeli ambalo zinashindwa kukidhi mahitaji yao pamoja na kuhalibika kwa kipindi kifupi.

“Kitendo cha baadhi ya watu wasio kuwa kuwa walwmavu kutengeneza  vifaa hivyo wanakuwa hawanaujuzi wakujua wanatakiwa wawekewe vitu gani ukiachana na sisi walemavu,” alisema Mdachi
Alisema mara kwa mara wamekuwa wakipokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya walemavu juu ya  ubora wa baiskeli hizo  wakiulizwa wanasema wanasema walizipata katika chama hicho jambo ambalo halina ukweli.

Afisa miradi wa  chama hicho Henry Chacha alisema  kuna watu wanachukua kazi za kutengeneza vifaa hivyo bila kuwa na taaluma nayo jambao ambalo linawasumbua walemavu wengi,
“Walemavu iliwaachane na kukaa mitaani na kuomba lazima wapate vifaa vya kuwa saidi ambapo unakuta wananunua vifaa hivyo kwa bei kubwa.”alisema Chacha
 Pia aliiomba serikali  kuwaongezea wataalamu katika chama hicho ilikupata  ubunifu zaidi wa kutengeneza vifaa  mbalimbali za walemavu.

No comments:

Post a Comment