Na. William Kange
Dar es salaam
Mchakato
wa zoezi la kuwasaka wachezaji wenye vipaji wakuli sakata kabumbu katika mchezo
wa soka la ufukweni “Beach soccer”
bado linazidi kushika hamasa kubwa huo ambapo zoezi hilo lahami kwa wachezaji
wenye vipaji waliopo mtaani kwa ngazi ya vilabu baada ya muda mrefu kuhusisha wanafunzi kutoka
vyuo mbalimbali kutoka Dar es salaam.
Akizungumza hii leo kwa njia simu na rise media kocha
mkuu wa timu ya taifa John Mwansasu
ameeleza kuwa bado tarehe rasmi ya kuanza mchakato wa zoezi hii haijawekwa wazi
kutoka na kukosa wadhami wakuweza kuendesha program ya kuwasaka wachezaji hao.
Amesema, kwa sasa wameamua kujidhatiti kutoka
wanafunzi vyuo muda mwingi wanakuwa kwenye masomo hivyo wanawakosa hususani wanapo
kabiliwa na maandalisi ya kujiandaa na mashindano mbalimbali ya kimataifa.
“punde
yatakapokuwa tayari tutawangazia kwasababu bado tunaongea na udhamini kwaajili
ya kuendesha program hii kwa ngazi ya vilabu kwa mkoa wa Dar es salaam”alisema mwansasu
Ameongeza
kuwa program hiyo yenye lengo la kuwasaka wachezaji watakao unda kikosi cha
timu taifa kwa mchezo huo ambapo pia wanatarajia kuwafikia wachezaji kutoka mikoa mbalimbali nchini
watakao kujakuwa msaada wa timu ya taifa kwa siku za usoni
“mchezo
huu unaitaji asili mali fedha hivyo yanahitajika maandalizi ya kutosha
ilikuusambaza mchezo huu kwa hapa nchini”alisema mwansasu
Tazama hapo chini kocha mkuu wa timu ya taifa John Mwansasu akielezea kuhusu mchakato wa kusaka vipaji vya mchezo wa mpira wa miguu wa ufukweni
Tazama hapo chini kocha mkuu wa timu ya taifa John Mwansasu akielezea kuhusu mchakato wa kusaka vipaji vya mchezo wa mpira wa miguu wa ufukweni


No comments:
Post a Comment