Wednesday, 12 July 2017

Usajiri wa Mbonde Simba ni Batiri - Kifaru

Na William Kange

Dar es Salaam

Uongozi wa klabu ya wakata miwa kutoka morogoro“ Mtibwa sugar” umesema hawautambui usajili wa beki wa kati wa klabu hiyo Salim Mbonde kwenda Simba kwa kuwa klabu hiyo imekiuka kanuni na utaratibu wa usajili kwani klabu Mtibwa bado inamkataba na mchezaji huyo.

Akizungumza na Rise Media msemaji mkuu wa klabu hiyo Thobias Kifaru ameutupia lawama uongozi wa klabu simba kwa kukiuka sheria na kanuni za kwakile kilicho onekana kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha beki wa kati wa klabu hiyo Salim Mbonde akimwaga wino kunako kablu hiyo.

“Bado haijawa rasmi na sisi tumesikia tu  tuna tegemea simba kujakufanya mazungumzo ndipo hapo mbonde atakapo tambulika mchezaji halali wa samba” alisema kifaru
Salim Mbonde akisaini kandarasi ya kuichezea klabu ya Simba 

Katika hatua nyingine Kifaru  amuzungumzia maandalizi ya Mtibwa Sugar kuelekea ligi kuu Tanzania bara ambapo klabu hiyo imeanza kambi yake hii leo Jiji Dar es salaam ambayo itadumu kwa wiki mbili itayomalizika July 29, na inatarajia kucheza mchezo wa mechi ya kirafiki dhidi ya Mbeya City itayopigwa kwenye uwanja wa Jamuhuri Mkoani morogoro

 “ kambi yetu itaanza julai 12 ampaka 29 ilikujiandaa na ligi kuu ilikujiimalisha tukiwa tuna malengo ya kuwa mabingwa kwa msimu wa mwaka 2017/2018”alisema kifaru
Kikosi Mtibwa Sugar msimu uliopita kikifanya mazoezi

Kipute cha ligi kuu Tanzania bara kinatajia kutimua vumbi mwezi ujao huku bingwa mtetezi akiwa ni Yanga akiwa amechukua  ubingwa mara 36, akifuatiwa na Simba ikiwa amechukua mara 18.

Tazama Kifaru akielezea usajili batiri wa Mbonde katika Klabu ya simba hapo chini


No comments:

Post a Comment